NILIFANYA MAPENZI NA MAITI 20 ILI NITAJIRIKE

NYEMO CHILONGANI
NILILALA NA MAITI 20 NITAJIRIKE
0718069269.

Sehemu ya Kumi na Nne.

“Imekuwaje tena?” nilijikuta nikimuuliza.
“kuwaje nini?”
“Kuwa humu!” nilimjibu.
“Hakuna kitu, kama bahati tumekutana tu,” aliniambia.
“Hapana! Kuna kitu.”
“Kipi hicho?” aliniuliza.
Kiukweli nilichanganyikiwa, mambo yaliyokuwa yakitokea baina yangu na huyu Majeed yalinishangaza sana, wakati mwingine nilihisi kabisa huyu jamaa alikuwa jini kwani kwa binadamu wa kawaida isingekuwa rahisi kiasi mhicho kwamba kila sehemu lazima tukutane.
Niliamua kuachana naye, safari ikaendelea, hatukuongeleshana japokuwa niliamini kila mmoja alikuwa na hamu ya kuongea na mwenzake. Mawazo yangu hayakutulia, nilianza kufikiria yale mambo yaliyotokea kipindi cha nyuma tangu nianze kuwa karibu na huyu Majeed.
Nilihisi kwamba inawezekana huyu jamaa alikuwa jini kwani isingekuwa kawaida kwa mtu wa kawaida kuwa katika hali ile. Nilibaki kimoya mpaka tulipoingia Uholanzi ambapo baadaye tukafika Dubai na kisha kuunganisha mpaka Tanzania.
Tulipofika Nairobi, hakuteremka, aliendelea kuwepo kwenye ndege mpaka tukaingia jijini Dar es Salaam. Tukateremka kutoka kwenye ndege na kwenda mpaka nje, alikuwa akiniangalia sana, tulipofika huko, nikaingia kwenye gari langu ambapo nilifuatwa na dereva.
“Unaondoka pasipo kuzungumza na mimi! Kweli mpenzi?” aliniambia huku akiwa ameegemea dirisha la gari, alikuwa nje.
“Ili?”
“Jamani! Hivi nimekufanyia nini tena? Mbona unakuwa hivyo?”
“Nipo vipi?”
“Hasira nyingi! Acha hizo mpenzi,” aliniambia.
Sikutaka kumsikiliza, unajua wakati mwingine unapoamua kufanya mambo yako hutakiwi kumsikiliza mtu yeyote yule, niligundua kwamba Majeed hakuwa mtu sahihi wa kuwa nami kwa sababu alikuwa mwingi wa hasira, nilitaka kubaki peke yangu na kama kutafuta mwanaume wa kunioa basi nitafute mbele kwa mbele.
Sasa wakati tunaondoka hapo uwanja wa ndege na kuangalia nyuma, niliona gari alilopanda yeye likiwa linatufuatilia kwa nyuma. Nilikasirika sana, nikamwambia dereva asimamishe gari, akasimamisha, nalo likasimama.
Nilichokifanya ni kuteremka kwa hasira, nikalifuata na kuomba nishushiwe kioo, akaanza kukishusha. Nilikuwa na hasira kali na muda huo nilidhamiria kumtukana ili kama mwisho, basi ajue huo ndiyo mwisho.
Kuna kitu kilitokea mpaka nilishangaa na hata leo ukiniuliza ilikuwaje, sijui chochote kile. Alipokishusha kioo na kumwangalia, nikashangaa hasira zote zikiyeyuka moyoni mwangu, furaha kubwa ajabu ikautawala moyo wangu, yeye mwenyewe akanirudishia na tabasamu pana.
“Nakupenda Majeed wangu,” nilimwambia huku nikimwangalia kwa matamanio.
“Najua mpenzi, hebu ingia ndani ya gari tuondoke.”
Kiukweli nilijishangaa sana, kwanza maneno hayo niliyotamka sikutaka kabisa kuyatamka ila nikashtukia nikiyatamka, hata kuingia ndani ya gari lile sikutaka lakini nikajikuta nikiingia bila kupenda.
Nilijishangaa sana, sikujua hasira zangu zote zilikwenda wapi na huyu Majeed alifanya nini. Kilichoendelea ni kumwambia dereva aelekee nyumbani kwani kulikuwa na sehemu nilipokuwa nikienda.
Nina uhakika kabisa kwamba siku hiyo akili yangu ilichukuliwa, sikumbuki njia tulizopita lakini ghafla nikakuta gari likiwa limesimama katika jumba kubwa sana, la kifahari ambalo kwa kuliangalia tu, isingekupa wakati mgumu kugundua kwamba mtu aliyekuwa akimiliki jumba hilo alikuwa mmoja wa watu wenye fedha nyingi sana hapa Tanzania.
“Karibu mpenzi,” aliniambia huku akinifungulia mlango.
“Hapa ni kwako?”
“Ndiyo! Karibu sana.”
“Mh! Unaishi na nani jumba lote hili?” niliuliza.
“Nipo na dada yangu tu.”
“Ni kuzuri sana,” nilimwambia, nilishindwa kuvumilia kabisa.
“Ila hapapashindi kwako! Ni pazuri zaidi ya hapa,” aliniambia huku akiachia tabasamu.
Tukatoka hapo, akanishika mkono na kuelekea huko ndani. Muonekano wake wa ndani ulinishangaza sana, ulikuwa ni wa kuvutia kupita kawaida, sebule nzima ilitawaliwa na harufu ya ubani iliyozichengua sana pua zangu.
Akaniambia nikae katika kochi wakati anakwenda kumuita dada yake ili aje kuniona. Wakati amekwenda huko, nilisikia akizungumza na mtu fulani huko, ila cha kushangaza, mtu huyo hakujibu, nilikuwa nasikia sauti ya paka tu, nikabaki nikijiuliza, je, Majeed alikuwa akizungumza na nani huko? Kama alikuwa dada yake aliyeniambia, mbona sikusikia sauti ya huyo dada zaidi ya sauti ya Majeed na sauti nyingine ya paka?
Wakati najiuliza hayo, Majeed akatokea, msichana aliyeongozana naye, sijui niseme nini. Nimezunguka Tanzania na kukutana na watu wengi, ila kwa uzuri aliokuwa nao huyu dada yake, hakika hakutakiwa kuishi katika dunia hii. Nikasimama kiadabu na kumsalimia, alipotaka kuitikia salamu yangu, nikashangaa akitoa sauti ya paka, nikashtuka na kubaki kutetemeka tu. Sikujua nini kilichokuwa kimemtokea.
****
“Mbona umeshtuka?” aliniuliza Majeed huku akiniangalia.
“Mbona ana sauti ya paka?” nilijikuta nimeuliza.
“Kwa sababu napenda paka wanavyolia. Wewe ndiye Zakia?” alinijibu dada yake na kunitupia swali.
“Ndiyo! Wewe je?”
“Mimi naitwa Nahlati,” alinijibu.
Sikuchoka kumwangalia, uzuri wake ulinifanya nimwangalie mara kwa mara, wakati mwingine nilitamani sana kuwa na uzuri kama aliokuwa nao Nahlati lakini ndiyo hivyo Mungu aliamua kunipa huu uzuri niliokuwa nao ambao kwa kifupi ulikuwa wa kawaida sana.
Tulikaa hapo sebuleni na kupiga stori za kawaida, baada ya hapo Majeed akaniomba niende chumbani kwake, hicho ndicho nilichokuwa nikikisubiria muda wote. Nilimpenda sana Majeed na kusema kwamba nimuache pasipo kufanya naye mapenzi kilikuwa kitu kisichowezekana kabisa.
Akanipeleka chumbani kwake, tofauti na nilivyofikiria, chumba kizima hakikuwa na kitu chochote zaidi ya kapeti la manyoya mengi. Nilishangaa sana kwani nilitegemea ningekuta kitanda cha gharama lakini matokeo yake ilikuwa tofauti kabisa.
“Eeh! Hujaweka hata kitanda,” nilimwambia huku nikionekana kushangaa.
“Sipendi kitanda wala godoro.”
“Hata kabati la nguo!”
“Hahaha! Tatizo lenu binadamu mnapenda sana kuweka vitu vingi chumbani,” aliniambia, jina lilelile aliloniita kipindi cha nyuma, akaniita tena, ila sikutaka kujiuliza kwani alikwishanipa majibu ya kuniita vile.
Nilianza kutembea huku na kule chumbani mule, kilikuwa kikubwa sana na kila nilipokuwa humo, nilitamani niendelee kuwa humo zaidi na zaidi. Moyo wangu ulipenda sana kuwa katika chumba kama hicho, wakati mwingine nilihisi kama nilikuwa katika sehemu fulani nzuri hata zaidi ya peponi.
Wakati nikiwa katika kutembeatembea, Majeed akatoka chumbani humo na kuelekea nje, sikujua alikwenda wapi, sikutaka kujali sana kwani humo ndani nilipokuwa, kulinipa amani ya moyo.
“Ni kuzuri mno, ni lazima Majeed anioe, haiwezekani kuachana naye,” nilijisemea huku nikitoa tabasamu pana.
Sikujua Majeed alikwenda wapi lakini baada ya kama nusu saa hivi, mlango ukafunguliwa na kuingia ndani. Alikuwa ameshika mfuko fulani mkubwa wa nailoni, ulionekana kuwa na vitu ndani yake lakini sikujua kulikuwa na nini.
Akanisogelea na kunipa huo mfuko ambapo baada ya kuangalia ndani, nikakutana na vitu mbalimbali kama manukato, nguo, viatu na mkoba mmoja mdogo.
Vitu vyote hivyo vilionekana kuwa na thamani kubwa, niliviangalia kwa makini, macho yangu yalikuwa yameduwaa, sikutaka kusubiri, hapohapo nikamsogelea zaidi na kumkumbatia, nilipotaka kuupeleka mdomo wangu mdomoni mwake, akanizuia.
“Nini tena jamani?” nilimuuliza kwa sauti tya mahaba ambayo niliamini ingemdatisha.
“Una haraka sana.”
“Jamani! Mbona unakuwa unaninyima sana uhuru! Unataka tuishi kama kaka na dada?” nilimuuliza, mwili wangu uliwehuka na kipindi hicho sikutaka kusikia lolote lile, nilitaka kufanya mapenzi tu.
“Punguza munkari mpenzi, mimi ni wako na wewe ni wangu,” aliniambia huku akinikazia macho.
Sikuwa na cha kufanya, kwa sababu aliniambia kwa maneno matamu kiasi hicho, nikaachana naye na kisha kuanza kuijaribu nguo iliyokuwa ndani ya mkoba ule, ilikuwa nguo nzuri ambayo iliendana sana na mwili wangu, mkoba ule ulinivutia sana.
“Nashukuru sana mpenzi,” nilimwambia.
Baada ya hapo, tukakaa chini na kuanza kuzungumza kama wapenzi. Kukweli siku hiyo nilimpania sana Majeed, nilimwangalia lakini akili yangu ilikuwa ikifikiria mapenzi tu.
Kuna kipindi nikawa namshika huku na kule kutaka kumuwehusha lakini wapi, nilijaribu utunduutundu wangu, mwisho wa siku nikachoka na kukaa kawaida tu na kupiga stori.
Ilipofika saa saba, wakati nasikia adhana ikiadhiniwa, usingizi mzito ukanikamata, nilijikaza nisilale lakini nikashindwa kabisa, nikajikuta nikilegea na kulala chini katika kapeti lile la manyoya. Kilichofuatia ni kuota ndoto.
Ndoto niliyoiota ni kwamba nilikuwa katika chumba kilichokuwa na harufu nzuri sana, sikujua kilikuwa chumba gani, wakati nimekaa nikijiuliza kuhusu chumba hicho, ghafla nikaona mlango ukifunguliwa na Majeed kuingia.
Kama ilivyokuwa siku nyingine, alikuwa akitabasamu, alionekana kuwa na furaha kubwa, akaanza kusogea kule nilipokuwa huku akivua nguo zake moja baada ya nyingine, aliponifikia, tayari alikuwa mtupu.
Akaanza kunishika huku na kule, nilihisi msisimko wa ajabu mwilini mwangu ambao sikuwahi kuupata kabla ya kipindi hicho, nilitetemeka sana, japokuwa mahali hapo kulikuwa na kiyoyozi lakini nilihisi kabisa kijasho chembamba kikianza kunitoka.
Nilimkumbatia kwa nguvu kama mtu ambaye hakutaka aondoke mikononi mwangu. Baada ya kuona kila kitu kimekamilika ndipo tulipoanza kufanya mapenzi hapohapo tulipokuwa.
Nilihisi hisia zote, nilijua kwamba nilikuwa nafanya mapenzi na Majeed lakini cha kushangaza baada ya dakika kadhaa, nikashtuka kutoka usingizini, nilikuwa ndani ya chumba cha Majeed, sikuwa na nguo hata moja mwili mwangu, wakati najiuliza ni kitu gani kimetokea, nikasikia sauti moyoni mwangu ikiniambia “Umefanya mapenzi na jini kwa mara ya pili, umeingia kwenye mtego wake, kujinasua ni mpaka rehema yangu itakapokushukia.”
NIKASHTUKA.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Jumapili.


Post a Comment

0 Comments